Na SGT Sophia Daniely- Singida
Sekretarieti ya bodi ya taifa ya Parole, ikiongozwa na Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza ( SACP )Lipiana Lyilo Januari 30,2026 imetoa mafunzo ya elimu ya Sheria ya Parole Mkoa wa singida,Maafisa Parole wa ngazi ya Wilaya pamoja na wakuu wa Magereza Mkoani humo.
Akizungumza katika mafunzo hayo,SACP Lyimo alieleza taratibu na vigezo vya utekelezaji wa Sheria ya Parole kuanzia ngazi ya kituo hadi taifa, akisisitiza umuhimu wa haki na uwazi katika upatikanaji wa wanufaika wa Parole.
Kwa upande wake , Mwenyekiti wa bodi ya parole Mkoa wa singida Bw Liana Hassan, ameshukuru ujio wa sekretarieti ya bodi ya parole taifa umewezesha bodi ya mkoa kutembelea wanufaika wa Parole na kujionea mabadiliko chanja ya kitabia.
Nae katibu wa parole Mkoa wa Singida , Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza( SACP) Khatibu Juma Semzono amesema mafunzo hayo yataongeza uelewa na ufanisi wa utekelezaji wa Sheria ya Parole kwa wajumbe na watendaji wa Parole ngazi ya mkoa na wilaya.
Mafunzo hayo yamelenga kuwajengea uwezo wajumbe wa bodi ya parole Mkoa, wakuu wa magereza na maafisa parole, Pamoja na kubaini changamoto zinazowakabili katika utendaji wa Majukumu yao.
Mwisho.





Post a Comment