Viongozi wa SMAUJATA wilaya ya Singida mjini wakiongozwa na Mwenyekiti MIRAJI HAMISI wamefanikiwa kunasa mtandao hatari ambao ukiwahusisha wanawake wanaoishi na watoto walioacha shule na kujiunga na makundi hatarishi.
Wakishirikiana na Dawati la Jinsia Wilaya ya Singida wanatarajia kuwarejesha watoto hao shuleni wiki ijayo sambamba na kuwanasua kutoka katika makundi hatarishi.
Akiongea na wahusika Mwenyekiti SMAUJATA Manispaa ya Singida Miraji amewaonya wanawake hao kuacha mara moja kuwarubuni watoto hao kuacha shule na kujihusisha na mambo ya mitaani.
"Acheni kuwafanyoa vitendo hivi watoto wetu ambao wana ndoto za kuwa viongozi wajao," Miraji.
No comments: