HII HAPA ILANI YA CCM 2025-2030 INAVYOWALENGA WATU WAKE



Na Amini Nyaungo



CHAMA CHA MAPINDUZI CCM KIMEANZISHWA 05,02,1977 ikiunganisha vyama viwili vya siasa TANU NA Afro-Shirazi Party (ASP) .

Viongozi wa vyama hivyo baada ya kuona umuhimu wa Demokrasia ndipo mfumo wa vyama vingi uliundwa mwaka 1992 na uchaguzi wake Mkuu umefanyika mwaka 1995.



Tangu kupata Uhuru na tangu Muungano wa Tanzania na Zanzibar hadi sasa CHAMA CHA MAPINDUZI ndicho kinaongoza dola.

Na desturi ya vyama vya siasa lazima kuwe na muongozo kwa kila baada ya miaka mitano ya uchaguzi mkuu.

ILANI ya CCM ya mwaka 2025 hadi 2030 ina vipaumbele vingi endapo watapata tenda ridhaa ya kuongoza nchi ikiwa uchaguzi mkuu unatarajiwa ulifanyika mwezi Oktoba mwaka huu.

Chamber Talk Show inakuletea vipaumbele 14 vya Ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2025-2030 kama amabvyo wamevieleza kupitia mkutano Mkuu uliofanyika mwezi Mae, 2025.

1. ARENA



Soko la ajira kwa vijana walio wengi hivi sasa wapo katika Sanaa mbalimbali ikiwemo burudani ya muziki hapa inajumuisha muziki wote iwe singeli, dance au bongo flava. Kupitia ilani ya Chama Cha Mapinduzi inasema kuwa kama watapata ridhaa watatengeneza ukumbi mkubwa wa burudani maarufu kama ARENA.

Rwanda ni sehemu nzuri ya mfano na wasanii wa hapa nyumbani wamekuwa wakililia juu ya hili msanii kama Ali Kiba Diamond wote wamekuwa wakihitaji jambo hili lifanyike.

Faida moja wapo ni mapato katika matumizi sahihi ya Ukumbi huo wa burudani mapato ya ndani na  nje ya nchi maana lazima itatumika katika matukio mbalimbali.

 

2. MAJI 90%



Ilani yao ya uchaguzi pia wamesema wata hakikisha kuwa asilimia 90 ya kaya zote zinafikiwa na huduma ya maji safi na salama. Kila mmoja anajua umuhimu wa kuwa na maji ya uhakika CCM wameiona hii na wamesema watahakikisha maji yanakuwa ya kutosha.

3. KUPUNGUZA BEI YA VIFAA UJENZI



Katika kuhakikisha kuwa wanaohitaji kujenga makazi yao hususani nyumba na sehemu ya biashara CCM wanasema watapunguza bei ya bidhaa vya ujenzi.

4. KUKAMILISHA MRADI WA MAJI



Wamesema kuwa watakamilisha miradi mikubwa ya maji katika miji 28 ili wananchi wake wanufaike na upatikanaji wa maji muda wote.

5. UJENZI WA BANDARI MPYA BAGAMOYO



Ili mapato yapatikane lazima kuwepo na bandari salama za kupakua mizigo bahati nzuri Tanzania tumejaliwa bahari hivyo moja ya mipango yao ni kujenga Bandari mpya ya Bagamoyo Mkoani Pwani.

6. UMALIZIAJI WA SGR



Tayari SGR imetufikia ikiwa kutoka DAR ES SALAAM hadi DODOMA sasa  ilani yao inasema kuwa watamalizia ujenzi wa SGR Kutoka DODOMA hadi MWANZA, pia kumalizaia ujenzi kutoka DODOMA , TABORA HADI KIGOMA.

7. UJENZI WA OFISI NA NYUMBA ZA WALIMU



CCM wamesema kuwa watahakikisha watajenga nyumba za walimu pamoja na ofisi zaa walimu nchi nzima ili walimu wawe katika wakati mzuri.

8. UNUNUZI WA NDEGE 8

Kuimarisha usafiri wa anga ilani ya CCM inasema wataongeza ndege nane mpya kwa ajili ya shirika la ndege ATCL.

9. AJIRA



Moja ya sehemu ambayo inashida ni ajira kwa vijana sasa CCM wameona lazima jambo hili liwepo ndipo wakasema watahakikisha watatoa ajira milioni 8.5.

 

10. KILIMO



Katika kilimo ambapo ndio sehemu sahihi na ajira nyingi zinatoka shambani wamesema kuwa eneo lla kilimo wataongeza eneo la kilimo cha umwagiliaji kufikia ekari milioni 5.

11. UMEME



Maendeleo ya nchi pia lazima kuwe na mwanga hapa sasa wametuambia kuwa watafanya usambazaji wa umeme kwa vitongoji vyote  nchi nzimaa ambapo kwa sasa kila kijiji kina umeme kilichobaki wamalizie ili wapate umeme katika vitongoji vyote.

12. MATREKTA



Uanzishwaji wa vituo vya Matreka na zana za kilimo kila kata hii ni moja ya mipango yao kuelekea 2025-20230.

13. BARABARA



Ujenzi wa barabara nne kutoka IGAWA- UYOLE, TUNDUMA yenye kilomita 218 pamoja na barabara ya Kibaoni , Majimoto- Inyonga KM 162 kuendelea na ujenzi wa Baravbara ya Geita- Bukoli-Kahama KM 133 lakini pia barabara ya Tarime- Mugumu km 87 pamoja na Barabara ya Mabokeni- Maramba-Bombo-Mtoni- umba hadi Same km 278.

14. MIKOPO



Ili kuhakikisha wananchi wake wanafanikiwa watahakikisha wanatoa mikopo kwa kampuni change na kazi za ubunifu.

Hii ndio ILANI YA CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) ikilenga kuimarisha watu wake wanao waongoza endapo watapata ridhaa.

Mwisho 

Post a Comment

Previous Post Next Post