ZIMAMOTO SINGIDA WAADHIMISHA SIKU YAO KWA KUWAKUMBUKA WALIOPATA AJALI KONA YA MOHAMEDI

Na Amini Nyaungo, Singida



Wananchi wameaswa kushirikiana kwa karibu na Jeshi la Zimamoto na Uokoaji wakati wote na hata yanapotokea majanga ya moto au maokozi ili jeshi hilo liweze kutoa msaada wake kama ilivyo adhima na lengo la Jeshi la Zimamoto.

Hayo yamefanyika leo (Mei 3,2025) na Jeshi la Zimamoto  Mkoani Singida walipokuwa wanashiriki zoezi la kufanya usafi katika makaburi yaliyopo  kona ya Mohamedi mkoani Singida ikiwa katika kuadhimisha wiki ya Zimamoto ambao katika makaburi hayo wahanga waliunguaa na moto kutokana na ajali ya gari mwaka 2007.



Akiongea na Chamber Media mara baada ya kufanya usafi katika eneo hilo Kaimu Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Singida Mrakibu Devotha Bigawa amesema kuwa wametumia wiki ya Zimamoto Mkoani Singida kushiriki katika shughuli za kijamii hususani kuwakumbuka waliowahi kupata ajali ya gari mwaka 2007 kona ya Mohamed ambao walikuwa 26.



“ Siku ya leo tumekuja kuwaenzi wenzetu waliotangulia mbele ya haki tupo maeneo haya kwa ajili ya kufanya usafi, tupo katika wiki ya Zimamoto ambayo imeanza April 28 na kuhitimisha Mei 4 mwaka huu, tumeamua kufika siku hii ya leo Jumamosi,”

 Ametumia nafasi hiyo kuwaasa  wananchi waweze kushrikiana kwa karibu na Jeshi la Zimamoto pindi wanapopata majanga ya moto ili waweze kusaidia kuokoa kama ambavyo ilivyo azma ya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji.



“Niwaase wenzangu pale unapoona kadhia yoyote inatokea piga 114 ili msaada wa haraka upatikane, hivyo tushirikiane,” Bigawa



Kwa upande wake Mwenyekiti wa Mtaa wa Kimpungua Jumanne Shabani Mahame amewashukuru Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kwa kufika na kuwakumbuka ndugu zao waliotanguia mbele ya haki kwa ajai hiyo.

“Kwa sasa tunayo namba 104 hivyo tukiona ajali tutapiga ili watusaidie tunawashukuru sana kwa ujio wenu hapa,” Jumanne

Aidha amesema kuwa ajali hiyo ilitokea tarehe 15,06,2007 eneo la kona ya Mohamed na watu 26 walipoteza maisha na kuungua moto hivyo kufanya wote kuzikwa eneo hilo.

Katika zaoezi hilo Jeshi la Zimamoto na Uokoaji waliambatana na Mabalozi wa Usalama Barabarani akiwakilishwa na Khadija Omary amesema kuwa wako tayari kutumika wakati wowote hivyo wamejisikia furaha kuungana na Jeshi la Zimamoto na Uokoaji.



“Tumefurahi kuungana na Jeshi la Zimamoto na Uokoaji sisi tupo tayari wakituhitaji tutafika kuungana nao na sisi tukiwahitaji tutawaomba ili tushirikiane,” Khadija.



Kwa upande wa  wananchi wa eneo hilo Jeni Shabani amesema hivi sasa wanaukaribu na watu wa usalama sio kama zamani hivyo kufika kwa jeshi la Zimamoto na Uokoaji ni sawa na kuzidisha ushirikiano

Mwisho 

Post a Comment

Previous Post Next Post