JESCA MAGUFULI AMPONGEZA RAIS DOKTA SAMIA, TIMBULO MSANII WAKE

  

Na Amini Nyaungo



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dokta Samia Suluhu Hassan amepongezwa na mtoto wa aliyekuwa Rais wa awamu ya tano Dokta John Pombe Magufuli ambaye ni Jesca Magufuli alipokuwa anaongea katika mahojiano na Millard Ayo.

Jesca amesema kuwa tangu kufariki kwa Dokta Magufuli Rais Dokta Samia Suluhu Hassan hakuwahi kuacha kuja kuwaona pamoja na kuwasomesha baadhi ya watoto ambao wanasoma chuo kwa kulipa ada.

Kupitia mahojiano hayo Millard Ayo amemuuliza Jesca kuwa Rais Dokta Samia amekuwa mtu wa faraja namba moja kwa Taifa je katika familia hiyo ilikuwaje ?

Jesca amesema kuwa “Mama amekuwa nasi tangia mwanzo nakumbuka hata kipindi mzee alipofariki baada ya kuapishwa alikuja nyumbani siku hiyo hiyo akamuahidi mama kuwa sitokuacha kama kuna changamoto zimetokea usisite kuniambia mdogo  wangu, kuanzia matibabu ya bibi yetu mama Samia aliendelea wale manesi hadi leo wapo wanaendelea kumuhudumia bibi, kipindi mzee anafariki sisi wengine tulikuwa tumeajiriwa kuna wadogo zetu walikuwa wanaasoma hadi sasa wanalipiwa ada ya chuo, na mengine mengi sio hayo tu siwezi kuyataja yote ila hayo ni machache,” Jesca



Jesca ameongeza kuwa Rais Samia ameweza kuendesha nchi vizuri kwani miradi mbalimbali ya maendeleo anaendelea kuimalizia ikiwemo Daraja la Kigongo Busisi.

Kwa upande wa timu gani anaipenda Jesca hajaweka wazi akisema kuwa hayati Dokta Magufuli alikuwa anapenda sana mifugo ila mpira sio sana huku miziki ndio alikuwa anasikiliza ikiwemo miziki ya zamani na ya sasa.



Jesca amesema msanii ambaye alikuwa anamsikiliza zaidi ni TIMBULO alikuwa namsikiliza sana.

“Kwenye mpira hapana ila miziki alikuwa anamsikiliza sana Timbulo, alikuwa anasikiliza nyimbo zake mno.

Jesca amesema msiba wa baba yake taarifa alipata kupitia mitandao kama wengine huku akihadithia maisha yake ya chuo hayajabadilika licha ya kuwa baba yake alikuwa Rais.

Mwisho 

Post a Comment

Previous Post Next Post