Na Amini Nyaungo
Aliyekuwa Mbunge wa Viti Maalum
Mkoa wa Singida kwa kundi la vijana Nusrat Hanje ambaye alikuwa Chama Cha
Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) atahamia Chama Cha Mapinduzi (CCM) kutokana
na kuunga mkono jitihada anazofanya Rais Dokta Samia Suluhu Hassan kuanzia sasa
hadi mwezi wa saba atahamia CCM.
HANJE ameyasema hayo leo katika
mkutano wa hadhara kwa wananchi waliokusanyika katika Wilaya ya Ikungi mkoani
Singida
Aidha katika moja ya
maneno yake amesema kuwa amegundua kuwa watu wanataka kutatuliwa shida zao hii
inatokana na uzoefu alioupata katika kipindi cha miaka mitano aliyokaa BUNGENI.
Katika hatua nyingine
amesema kuwa Rais Dokta Samia anafanyakazi nzuri halali usiku na mchana hivyo
ni vyema akahamia CCM muda mchache ujao kutokea sasa hadi mwezi was aba.
“katika Tanzania na Mkoa wa
Singida mama anapambana kinomanoma, mama anapambana anapiga kazi usiku na mchana,
nimeamua mwenyewe bila ya kulazimishwa mwenyewe kwamba muda wowote kutokea hivi
sasa hadi mwezi was aba nitahamia CCM,”Hanje
Katika Mkutano huo pia
Hanje amewataka wanaikungi kujitokeza kwa wingi kumuunga mkono kuhamia CCM kwa
kuwa tayari changamoto zao na kero zao zinaweza kutatuliwa bila kusababisha
vurugu wala machafuko.
Mwisho

Post a Comment