MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI AWAPA HABARI NJEMA YA KISHERIA SINGIDA

 

Na Amini Nyaungo



Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Hamza Johari amesema kuwa jopo la wanasheria waliofika Mkoani Singida watasaidia wananchi mbalimbali watakaokuwa na shidaa za kisheria kwa siku saba ambapo leo ndio ulikuwa uzinduzi wake Stendi ya zamani Mkoani Singida. 

Hayo ameyasema leo katika uzinduzi wa Kisheria uliofanyika Stendi ya zamani ya Mabasi Mkoani hapa.

Katika hotuba yake Mhe. Hamza amewataka wananchi kutumia vizuri siku saba ili waweze kunufaika kwa kutatua shida mbalimbali za kisheria zinazowasibu.

“Niwaase watumie vizuri siku hizi Mwanasheria Mkuu wa Serikali yupo muitumie vizuri, ambapo hii inafanyika bure,” Hamza



Aidha Mwanasheria Mkuu wa Serikali amesema kuwa baada ya uzinduzi wa kamati hiyo utafuatiwa na Kliniki ya sheria kuanzia leo (Mei 19,05,2025 hadi  25,05,2025) kutakuwa na huduma za kisheria zitatolewa  kwa wananchi bila malipo yoyote.

Amesema kliniki hizo za kisheria zinaratibiwa na kusimamiwa na ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali  ni utekelezaji wa ibara ya 8 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  ambapo inaeleza jukumu la serikali la kuwajibika kwa wananchi.



Pia amesema kuwa huo ni utekelezaji wa maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ambapo amekuwa akiwaeleza viongozi mbalimbali katika kutatua kero za wananchi na kuzipatia ufumbuzi.

Katika kliniki hizo zitalenga mambo kadhaa ambayo ni pamoja na Kusogeza huduma za kisheria karibu na wananchi,kuwaongoza wananchi katika taratibu za kupata haki zao pale zinapovunjwa pamoja na kutoa elimu ya kisheria  kwa wananchi na kuongeza ushrikiano.



Kwa upande wa mgeni rasmi ambaye ni Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mhe. Halima Dendego yeye amezindua rasmi Kamati ya Ushauri wa Kisheria ngazi ya mkoa na wilaya pamoja na kliniki ya sheria bila malipo kwa wananchi.

Amesema kuwa “ mpango huu unalenga kusaidia wananchi wenye changamoto mbalimbali za kisheria kwa kuwapatia msaada wa kitaalamu bila gharama kama ambavyo Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan imekuwa ikielekeza,” Dendego

Mwisho

 

Post a Comment

Previous Post Next Post