Na Jumbe Ismailly SINGIDA
SHIRIKA la Kimataifa
lisilo la kiserikali (NGO) la Sightsavers Mkoani Singida limewapatia watu 1,830
wenye kukabiliwa na changamoto ya uoni pamoja na huduma ya upasuaji mdogo wa
motto wa jicho na kufanikiwa kuchangia kuondoa upofu unaoweza kuzuilika kwa wananchi
wa Mkoa huo.
Akitoa taarifa za mradi
huo ulianza kutekelezwa katika Halmashauri saba za Mkoa wa Singida tangu mwaka
2023,Mratibu Mradi, Sightsavers Mkoa ni Singida,Upendo Minja alifafanua zaidi
ya watu 1,230 wenye changamoto ya uoni walipatiwa huduma za upasuaji mdogo wa
mtoto wa jicho na zaidi ya watu 600 walipatiwa huduma ya miwani ili kurekebisha
uoni wao.
Hata hivyo Upendo aliweka
wazi kwamba kupitia utekelezaji wa majukumu yake, shirika hilo limeweza
kuhamasisha jamii pamoja na viongozi kuhusu umuhimu wa huduma za afya na haki
za watu wenye ulemavu na umuhimu wa ushirikishwaji wao katika maendeleo
yaTaifa.
“Kwa wenye changamoto za
uoni,watu zaidi ya 600 wamepatiwa huduma ya miwani ili kurekebisha uoni wao
sambamba na huduma hizo vile vile zaidi ya watu 1,230 wamepatiwa huduma ya
upasuaji mdogo wa motto wa jicho na kufanikiwa kuchangia kuondoa upofu unaoweza
kuzuilika kwa wananchi wa Mkoa wa Singida”alisisitiza Mratibu huyo wa mradi.
Mratibu huyo wa mradi
alibainisha kwamba shirika hilo linafanyakazi na serikali, mashirika ya kiraia
pamoja na jamii ili kuboresha huduma za afya ya macho, kuwezesha watu wenye
ulemavu kupata haki zao na kusaidia maendeleo ya kiuchumi.
Hata hivyo Upendo aliweka
wazi kwamba kupitia utekelezaji wa majukumu yake, shirika hilo limeweza
kuhamasisha jamii pamoja na viongozi kuhusu umuhimu wa huduma za afya na haki
za watu wenye ulemavu na umuhimu wa ushirikishwaji wao katika maendeleo
yaTaifa.
Aliweka bayana kuwa
katika kutekeleza jitihada za maendeleo kwa wananchi, Mkoa wa Singida chini ya
serikali ya awamu ya sita ya Mama Samia Suluhu Hassani umeweka mazingira
wezeshi kwa wadau kuweza kutekeleza miradi ya maendeleo ya Mkoa wa Singida.
“Mmoja wa wadau
wanaoshirikiana na Mkoa wa Singida ni shirika la Sightsavers lenye dhima ya
kutoa huduma endelevu za afya ya macho kwa wananchi na kutetea haki ujumuishi
wa watu wenye ulemavu katika Mkoa wa Singida” alisisitiza mratibu mradi huyo.
Hata hivyo aliweka bayana
kwamba kutokana na mazingira hayo wezeshi, Sightsavers husaidia kufanikisha
huduma za afya ya macho kwa watu walioko vijijini pamoja na maeneo ya pembezoni
ili kufikia adhima ya serikali ya huduma bora za afya.
Kwa mujibu wa mratibu
mradi huyo katika kipindi cha miaka mitatu ya Mheshimiwa Raisi Daktari Samia
Suluhu Hassani,Shirika hilo la Sightsavers kuanzia mwaka 2023 mpaka sasa
linaendelea kutekeleza mradi wa Macho Yangu katika Halmashauri saba za Mkoa wa
Singida.
Alifafanua kuwa mradi huo
umeweza kufikia wananchi katika utoaji wa huduma za upimaji na uchunguzi wa afya
ya macho,utoaji huduma za miwani kwa lengo la kurekebisha uoni pamoja na
upasuaji mdogo wa motto wa jicho.
“Takwimu zinaonyesha watu
zaidi ya 18,000 wamepata huduma ya uchunguzi wa macho kupitia vituo mbali mbali
vya afya pamoja na huduma mkoba zinazofanywa kwa ajili ya kusogeza huduma
karibu zaidi na wananchi.
Aidha Upendo alibainisha
kuwa katika utekelezaji wa mradi wa uboreshaji wa uchumi kwa watu wenye
ulemavu,Shirika la Sightsavers kwa kushirikiana na Mkoa limefanya hamasa kwa
watu wenye ulemavu kujiunga na shughuli za kilimo cha mtama, kufanya mafunzo ya
ujasiriamali na kujiajiri, hususani kwa vijana.
Alifafanua pia kwamba
idadi ya vijana wapatao 50 kutoka sehemu mbali mbali za Mkoa wa Singida
wamepatiwa mafunzo ya ujasiriamali na kujiajiri na watu wenye ulemavu wapatao
30 wamepatiwa mafunzo ya kilimo bora cha mtama katika Halmashauri ya wilaya ya
Mkalama.
Hata hivyo Upendo aliweka
bayana pia kuwa ili vijana pamoja na watu wenye ulemavu wawezeshwe kushiriki
katika kuchangia shughuli za kiuchumi, Sightsavers waliweza kugawa vifaa
saidizi kulingana na mahitaji kwa watu wapatao 11 na kuchangia mitaji kwa vijana
watano wenye ulemavu kwa kuwapatia vifaa vya kuongeza mitaji yao.
Alivitaja vifaa hivyo
kuwa ni pamoja na mitungi ya gesi, mashine ya kushonea, masweta, cherehani
pamoja na bidhaa za dukani kama chachu ya kuhamasisha wadau wengine kuweza
kufanya kazi na makundi hayo maalumu.
MWISHO.

Post a Comment