Na Jumbe Ismailly SINGIDA
HALMASHAURI ya wilaya ya
Singida inatarajia kutumia shilingi milioni 17,705,174,240/= kukamilisha ujenzi wa bwawa la umwagiliaji
katika Kata ya Msange,wilayani Singida
lenye ukubwa wa hekta 1,000.
Akielezea mafanikio ya
Idara ya Kilimo,Mifugo na Uvuvi kwa kipindi cha mwaka wa fedha wa 2021/2022
hadi mwaka 2023/2024, Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Singida,Elia
Mlangi Digha alisema Halmashauri hiyo inajihusisha na kilimo cha umwagiliaji
kinachofanyika katika maeneo yenye mabonde na maeneo yanayofaa kwa ajili ya
kilimo cha kumwagilia.
Aidha Digha ambaye pia ni
diwani wa Kata ya Msange alifafanua kuwa wataalamu wa umwagiliaji walibaini
maeneo yanayofaa kwa kilimo cha umwagiliaji yenye ukubwa wa hekta 5,157
yanayofaa kwa uchimbaji wa visima kwa lengo la kufanya shughuli za kilimo,
hususani wakati wa kiangazi.
Akifafanua zaidi
Mwenyekiti huyo alisema katika kipindi cha miaka mitatu serikali pia
imeidhinisha ujenzi wa mabwawa ya umwagiliaji katika kata ya Mughamo na Msange.
“Halmashauri imewezeshwa
ujenzi wa bwawa la umwagiliaji katika Kata ya Msange ambapo eneo la umwagiliaji
lina ukubwa wa hekta 1,000 na mradi unagharimu jumla ya shilingi
17,705,174,240/= ambapo shughuli za ujenzi zinaendelea.
Akizungumzia usajili wa
wakulima kwenye mfumo wa TFRA,Digha aliweka wazi kwamba Halmashauri ya wilaya
ya Singida imefanikiwa kusajili kwenye daftari wakulima 42,766 na kuwaingiza
kwenye mfumo wa TFRA wa mbolea za ruzuku ili kuhakikisha wanapata namba za kuwawezesha
kupata mbolea na mbegu za ruzuku.
“Halmashauri ilikuwa na
lengo la kusajili wakulima 42,766 kutoka katika vijiji vyote 84,hadi sasa
tumesajili wakulima wote kwa asilimia 100 na zoezi la usajili
linaendelea”alisisitiza Mwenyekiti huyo wa Halmashauri ya wilaya ya Singida.
Halmashauri ya wilaya ya
Singida ina eneo la kilomita za mraba 5,053 ambazo kati ya hizo,eneo linalofaa
kwa kilimo ni kilomita za mraba 3,214 na kilomita za mraba 1,839 zinazobaki ni
kwa ajili ya eneo la malisho,misitu,maji,maziwa na mito na eneo kwa ajili ya
madini,vilima pamoja na mawe.
MWISHO.


Post a Comment