IDADI YA WAFUNGAJI NYUKI MKOA WA SINGIDA YAFAHAMIKA WANAUME WAONGOZA

 Na Jumbe Ismailly SINGIDA

 


MKOA wa Singida una jumla ya wafugaji nyuki 15,326 wakiwemo wanaume 12,377 na wanawake 2,949 wanaozalisha zao la asali katika mapori na misitu iliyopo katika Halmashauri saba zilizopo katika Mkoa huo.

 

Afisa Maliasili wa sekretarieti ya Mkoa wa Singida,Charles Kidua alitoa takwimu hizo alipokuwa akitoa taarifa ya mazao yanayotokana na nyuki katika Mkoa wa Singida.

 

Aidha afisa huyo mwenye dhamana ya kusimamia sekta ya maliasili alifafanua kwamba Halmashauri ya Itigi inaongoza kwa kuwa na wafugaji 5,012 wakiwemo wanaume 4,030 na wanawake 982.

 

Kwa mujibu wa Kidua Halmashauri ya wilaya ya Ikungi ina wafugaji nyuki 3,841 wakiwemo wanaume 2,636 na wanawake 1,205 wakati Halmashauri ya wilaya ya Manyoni ina jumla ya wafugaji nyuki 1,934 wakiwemo wanaume 1,876 na wanawake 78.

 

Hata hivyo afisa maliasili huyo alibainisha pia kuwa Halmashauri ya wilaya ya Iramba ina jumla ya wafugaji nyuki 1,562 wakiwemo wanaume 1,241 na wanawake 321 na Halmashauri ya wilaya ya Singida ina jumla ya wafugaji nyuki 1,232 wakiwemo wanaume 1,016 na wanawake 216.

 

Kwa upande wa Halmashauri ya Mkalaama ina jumla ya wafugaji nyuki 905 wakiwemo wanaume 812 na wanawake 93 na Halmashauri ya Manispaa ya Singida ina jumla ya wafugaji nyuki 820 wakiwemo wanaume 766 na wanawake 54 na kuzitaja wilaya zenye vituo vya kusindika asali kuwa ni wilaya ya Singida na wilaya ya Manyoni.

 

“Wilaya zenye kituo cha kusindika asali ni wilaya ya Singida yenye viwanda viwilio kikiwemo cha SIDO Mkoa,Kijiji cha nyuki kilichopo Kijiji cha Kisaki,Manispaa ya Singida na wilaya ya Manyoni kiwanda cha Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania(TFS)”alisisitiza Kidua.

 

Akizungumzia soko la asali inayopatikana Mkoa wa Singida,Kidua alisema kwamba asali hiyo huuzwa katika mikoa ya Manyara,Arusha,Dodoma pamoja na mkoa wa Dar-es-Salaam.

 

MWISHO.

Post a Comment

Previous Post Next Post