UCHAGUZI MKUU 2025 UPO PALEPALE, “NO REFORM” WAANGALIE KATIBA


Na Amini Nyaungo

Uchaguzi mkuu wa Tanzania wa kuchagua Rais,Wabunge,Madiwani unaotarajiwa kufanyika mwezi Oktoba mwaka 2025 utakuwepo na utafanyika kama ambavyo ulivyopangwa kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inavyotaka.
Hayo ameyasema Mkuu wa Wilaya ya Manyoni Mhe. Vicent Mashinji (March 10,2025) akiwa moja ya wageni wakati wa mafunzo yaliyotolewa na Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Singida Martha Gwau alipokuwa anatoa mafunzo kwa Umoja wa Wanawakewa Wilaya ya Manyoni(UWT) ambapo aliwaleta watalaamu mbalimbali kutoa mafunzo hayo, ambapo DKT. Mashinji ametanabaisha  kuwa uchaguzi mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambao umepangwa kufanyika  utakuwepo kama amabavyo ulivyopangwa kwa  mujibu wa sheria na katiba ya nchi.
DKT. Mashinji amesema katiba inaweka wazi kuwa kila ifikapo miaka mitano na Jumapili ya kila mwisho ya mwezi Oktoba katika hiyo miaka mitano kunahitajika kufanyike uchaguzi mkuu na ndivyo ilivyo mwaka huu, hivyo kawaambia wananchi wa Manyoni wasiwe na wasiwasi kila kitu kitaenda kama kinavyohitajika.

“Naomba niwatoe wasiwasi uchaguzi mkuu mwaka huu utakuwepo kama kawaida kama katiba inavyosema, waambieni wakaangalie Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inavyosema, hivyo uchaguzi utakuwepo kama kawaida,” DKT. Mashinji.

Tanzania inafanya uchaguzi kila baada ya miaka mitano kwa ajili ya kuchagua Wabunge, Madiwani pamoja na Rais.

Mwisho 

Post a Comment

Previous Post Next Post