NGUSHI AFUNGUA PAZIA, TAKWIMU ZA RAUNDI YA KWANZA NBC


Na Amini Nyaungo



Nyota wa Mashujaa FC inayoshiriki ligi kuu Tanzania Bara Chrispin Ngushi ndiye mfungaji wa goli la kwanza ligi kuu Tanzania Bara iliyoanza kutimua vumbi Agusti 16,2024 ambapo yeye amefungo goli hilo tarehe 17.08.2024 Mashujaa walipowafunga Dodoma Jiji 1-0, katika uwanja wao wa nyumbani wa Lake Tanganyika mkoani Kigoma.

Ngushi alifunga goli  la kufungua pazia la msimu dakika ya 35 ya mchezo huo na kuandika historia ya kufunga goli la kwanza la mashindano hayo ambapo bingwa mtetezi klabu ya Yanga yenye maskani yake Twiga na Jangwani pale Kariakoo Dar es Salaam.



Ngushi aliwahi kucheza Mbeya kwanza kwa mafanikio makubwa kwa kufunga magoli na kuisaidia timu yake kupata alama nyingi wakati huo na kusababisha kusajiliwa na Yanga.

Baadae akapata nafasi ya kucheza Yanga ambapo hakupata nafasi akatolewa kwa mkopo Coastal Union na msimu huu anautwanga mashujaa

Mchezo wa ufunguzi Tanzania Prison dhidi ya Pamba uliopigwa tarehe 16. 08.2024 ulitoka sare ya bila kufungana.



Katika hatua nyingine raundi ya kwanza yamefungwa magoli 14 mchezo ambao umetoa magoli mengi ni ule wa Ken Gold dhidi ya Singida Black Stars ambao umetoa magoli 4, Singida wakiondoka na ushindi wa magoli 3-1 ugenini.

Katika magoli 14 , magoli saba (7) yamefungwa kipindi cha kwanza huku (7) mengine yamefungwa kipindi cha pili.

Ligi hiyo kwa sasa ipo raundi ya 22 na kupitia Chamber Media tutakuandalia magoli yote yaliyofungwa katika raundi zote.

Mwisho 

Post a Comment

Previous Post Next Post