SOWAH ASEMA AZIZ KI NI HATARI, ANAPENDA UGALI,WALI MAHARAGE

 

By Amini Nyaungo



Mshambuliaji wa Singida Black Stars Jonathan Sowah ameweka wazi kuwa kiungo wa Yanga Azizi KI moja ya wachezaji bora ndani ya ligi kuu ya soka ya Tanzania Bara kwakuwa anamjua tangu walipokuwa wanacheza ligi moja nchini Ghana.

Amesema hayo jana akiwa na Waandishi wa Habari( Media Day) Singida Black Stars walipokuwa na siku yao ya waandishi wa habari kama bodi ya ligi inavyoelekeza vilabu vyote viwe na siku maalumu kwa ajili ya waandishi wa habari kuwauliza mawali wachezaji na viongozi wa imu husika.



Amesema kuwa kama atacheza na Ki atafunga magoli mengi sana kutokana na ubora wa pasi za mwisho za nyota huyo wa Yanga.



“Azizi Ki ni rafiki yangu tumecheza wote ligi moja nchini Ghana namjua ni mchezaji mzuri sana kwa ubora aliye nao, kama ningecheza naye timu moja ingekuwa hatari sana,” Sowa

Pia amesema kuwa ligi ya Tanzania ni nzuri na ina ushindani sana ana wakaribisha wachezaji wengine waje waone ubora wa ligi hii.

“Nafikiri ni ligi nzuri sana kuna ushindani wa hali ya juu sana wachezaji wengi waje hapa,” Sowah

Sowah amesema kuwa chakula anachokipenda akiwa nchini Tanzania ni Wali Maharage au Maharage na Ugali.

“ Chakula kizuri wali na mahaarage au mahaarage na ugali,” Sowah

Nyota huyo amefunga magoli 7  ya Ligi kuu na amesajiliwa dirisha dogo la ligi bado ligi inaendelea huenda akafunga mengi Zaidi.

Mwisho 

Post a Comment

Previous Post Next Post