SIRI YA USHINDI CCM WILAYA YA IKUNGI YAFICHUKA

 Na Amini Nyaungo

Kazi nzuri na maneno yanayojenga ndio sababu ya ushindi iliyoupata Chama cha Mapinduzi (CCM) Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi mkoani Singida.

Hayo yamesemwa leo na Katibu wa CCM Wilaya ya Ikungi Joshua Mbwana Hungura alipokuwa anaongea na Waandishi wa Habari katika ofisi za Chama Cha Mapinduzi(CCM) zilizopo wilayani hapa.
Hungura amesema kuwa CCM  imefanikisha miradi mingi ya maendelo ndani ya Wilaya hiyo ikiwemo Shule, Barabara pamoja na Umeme hivyo wananchi wapo makini na kuona namna gani chama hicho kinafanyakazi yake vizuri.

"Mwaka huu wa 2024 tulifanya kampeni kwa kuonyesha miradi ambayo CCM wamewaletea wananchi wake pamoja na maneno kidogo tu na ndio sababu ya sisi CCM kushinda kwa kishindo hivyo yoyote akitaka kuhoji au kuuliza juu ya ushindi wetu waambieni hivyo," Hungura.
Aidha katika hatua nyingine Hungura amesema kuwa matokeo hayo ya uchaguzi wa serikali za Mitaa ndio ambavyo itakuwa katika uchaguzi mkuu ujao wa mwaka 2025.


Hungura ameweka wazi kuwa CCM kitendelea kushikamana na kutekeleza Ilani yake ili kuwaletea wananchi maendeleo

Post a Comment

Previous Post Next Post