HABARI PICHA : MIAKA 63 YA UHURU WA TANGANYIKA, SINGIDA GUNTO

Leo ni maadhimisho ya miaka 63 ya Uhuru wa Tanganyika ambapo mkoa wa Singida iliadhimisha kwa kupanda miti katika Hospitali ya mkoa wa Singida na sehemu mbalimbali.

Viongozi mbalimbali walikuwepo akiwemo Mkuu wa mkoa wa Singida Halima Dendego, Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Singida Martha Mlata , Godwin Gondwe Mkuu wa Wilaya ya Singida na viongozi wengine pamoja na Wananchi.
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Singida Martha Mlata akiwa katika zoezi la upandaji miti katika kuadhimisha miaka 63 ya Uhuru wa Tanganyika.

Mkuu wa Wilaya ya Singida Godwin Gondwe akiwa katika zoezi hilo la upandaji miti katika kusherehekea Uhuru miaka 63.
Jamii mbalimbali zikijumuika katima zoezi la upandaji wa miti mkoani Singida
Watu wamejitokeza kupanda miti mkoani Singida katika kusherehekea miaka 63 ya Uhuru
Zoezi lilihudhuliwa na viongozi wa kisiasa pamoja na Wananchi mbalimbali
Wananchi wakiendelea kupanda miti katika siku ya sherehe ya miaka 63 ya Uhuru
Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa Mkoa wa Singida  wa Chama cha Mapinduzi (UWT) Martha Kayaga naye alikuwepo katika upandaji wa miti
Mhe. Godwin Gondwe akiwa katika harakati za kupanda miti

Wananchi nao wakiwa katika sehemu ya ya upandaji wa miti
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Singida Yagi Kiaratu akiwa katika shughuli ya upandaji wa miti.

Photo Credit: SNADA REAL ONLINE TV

Post a Comment

Previous Post Next Post