Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko amewahimiza wanawake nchini kutumia fursa ya mifuko ya uwezeshaji wananchi kiuchumi kwa ajili ya kukopa na kujiongezea vipato.
Dkt. Biteko ametoa rai hiyo mkoani Singida wakati akimwalilisha Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa kwenye Kilele cha Maonesho ya Saba ya Mifuko na Programu za Uwezeshaji kwa Mwaka 2024.
Dkt. Biteko amebainisha kuwa Rais Dkt. Samia alitoa wito kwa benki kuongeza kiwango cha kutoa mikopo kwa wananchi huku akitolea mfano Benki ya Maendeleo ya Kilimo (TADB) ambayo mwaka 2020 ilitoa shilingi bilioni 63 na hadi kufikia Agosti 2024 imetoa mikopo kiasi cha shilingi bilioni 337.
Sambamba na hayo Dkt. Biteko amezindua Mwongozo wa Uratibu na Usimamizi wa Mifuko na Programu za Uwezeshaji ili iwe nyenzo ya kuimarisha utendaji wa mifuko na programu za uwezeshaji kwa lengo la kuondoa changamoto zilizopo hasa mikopo chechefu ili kufikia malengo yaliyokusudiwa katika kukuza uchumi na kupunguza umaskini katika jamii.
Mwisho
No comments: