HABARI

MICHEZO

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

HABARI

HABARI

MAKALA

» »Unlabelled » AKITOKEA KIONGOZI ASIYE NA FEDHA ANA SERA NZURI MCHAGUENI-BITEKO


Na Amini Nyaungo
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dokta Dotto Biteko amewaomba wananchi wa Singida kuchagua viongozi walio na sifa ambao wataweza kuweka msingi imara wa uongozi na kuwaletea maendeleo.

Biteko ameyasema hayo leo katika Maonyesho ya Saba ya Uwezeshaji yaliyofanyika mkoani Singida ambapo yeye amemuwakilisha Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.

"Chagueni viongozi walio na sera nzuri zitakazoweza kutatua shida zenu, msichague viongozi kwa urafiki na wasiokuwa na sifa'" Biteko
Ametoa wito kwa Benki zote kuwaamini wanawake katika utoaji wa mikopo ili iwasaidie katika shughuli zao anaamini wanawake wanaweza kuzilinda familia.

" Nitoe wito kwa Benki zote wawape kipaumbele wanawawake katika kuwakopesha fedha ili walete maendeleo," amesema

Pia amezindua Muongozo wa Mifuko na Program za Uwezeshaji wananchi pamoja na kutoa vyeti kwa makundi mbalimbali.

 Biteko hakuacha kumpongeza mkuu wa mkoa wa Singida Halima Dendego kwa kazi nzuri aliyoifanya kuandaa maonyesho  haya.
Amewaomba wananchi wa Singida kupendana akieleza kuwa endapo wanapenda uchumi utakua na maendeleo yatakuwepo.

Mwisho

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply