HABARI

MICHEZO

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

HABARI

HABARI

MAKALA

» » VIJANA WAILINDE AMANI YA TANZANIA -ZANURA

Na Amini Nyaungo

Vijana wametakiwa kuwa wamoja na kulinda amani ya nchi ya Tanzania kwa kuungana kwa pamoja ili waimarishe undugu pamoja na vuguvugu la kujitolea ii kuleta mapinduzi ya kifikra kwa jamii pamoja na kuhimizana fursa mbalimbali katika jamii.
Hayo ameyasema leo Katibu  wa Taifa letu  Kesho yetu Movement maarufu kama (TK Movement) Zanura Adam walipokuwa wanazindua kampeni hiyo kata ya Merya Mkoa wa Singida ambapo mgeni rasmi alikuwa Diwani wa kata hiyo Iddi Rajabu akimuwakilisha Mwenyekiti wa CCM Halmashauri ya Mnaipsaa ya Singida Vijijini Elia Digha.
Zanura amesema lengo la TK Movement  kuendelea kuwaunganisha vijana na hawafungamani na mtu au chama chochote dini au kabila hivyo yoyote anakaribshwa.

“TK Movement ipo kwa ajili ya kuleta mapinduzi ya kifikra katika jamii, haifungamani na mtu yoyote, dini, chama au kabila,”Zanura

Zanura amewaomba vijana kuungana na TK Movement ili waweze kuwa pamoja , amesema kitaifa ilizinduliwa tarehe 25.05.2024 huku kwa mkoa wa Singida ilizinduliwa tarehe 20.07.2024 kwa  upand wa wilaya ya Singida vijijini imezinduliwa 31.08.2024 leo hii wamezindua katika kata ya Merya.

Kwa upande wake mgeni rasmi wa tukio hilo Diwani wa kata ya Merya Iddi Rajabu amewaomba vijana kubadili na kumrudia Mungu ili kuweza kuondoa mambo ya ajabu yanayoendelea hapa nchini.

Rajabu amesema ni lazima vijana wawe tayari kubadilika na kuwa na hofu ya Mungu ili kila kitu kiwe katika mstari uliokuwa mzuri.
“Vijana wanatakiwa wabadilike wawe katika mstari mzuri wakifanya hivyo kia kitu kitakuwa sawa , wazazi wapeekeni watoto katika mafunzo ya kiimani ili wawe watoto wema,” Iddi.

 Mwisho

«
Next
This is the most recent post.
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply