Na Amini Nyaungo
Bure amewaambia wanafunzi hao kuwa maendeleo ya nchi hii yanatokana na ustawi bora wa Chama Cha Mapinduzi na viongozi wake wanaoongoza nchi.
Aidha katika ufunguzi wa tawi hilo amewaomba vijana kuchukua fomu kwa ajili ya uchaguzi kama wanaona wanavyo vigezo, ameainisha ya kuwa katika uchaguzi ujao fomu ya Rais ndio pekee itakuwa moja lakini zingine zote zinatakiwa vijana wachukue kwa ajili ha kuomba nafasi mbalimbali.
Katika tawi hili Bure ameomba wapatikane viongozi wa tawi ambapo Mwenyekiti, Katibu pamoja na Hamasa wameweza kuchaguliwa baada ya kikao hicho wamepata nafasi ya kushukuru kwa kupewa nafasi hiyo na kuahidi kukuza na kuendeleza mazuri ya Chama cha Mapinduzi.
Mwisho.
Post a Comment