Hanje amesema kuwa yeye ni miongoni mwa Wabunge wanaounga mkono harakati za Rais Samia anazoendelea kuzifanya katika kuwakomboa vijana na wananachi wake.
Wakati anakabidhi Mifuko hiyo ya cementi ameweka wazi kuwa ataendelea kushirikiana nao vijana katika kila zuri watakalolifanya ili mradi waendelee kufanikiwa katika maisha yao.
"Tutaendelea kushirikiana katika mambo mbalimbali kama kuna jambo zuri tutashirikiana ili tija upatikane," Hanje.
Hanje ametumia nafasi hiyo kuwaomba vijana kubuni mbinu mbalimbali zitakazoweza kuwaletea maendeleo pamoja na kipato ili waendeleze familia zao.
"Jitahidi kubuni miradu utakayoweza kuwasaidia kiuchumi kama ambavyo mradi huu unafanyakazi, " Hanje.
Aidha Mbunge Hanje amewapa nauli vijana zaidi ya 200 ambao walimaliza na kufunga kambi yao ikiwa na lengo la kuwafikisha majumbani mwao.

Mwisho
Post a Comment