PANDAUYAGA AWAACHA MBALI WAPINZANI UDIWANI NDEVELWA


Msimamizi wa uchaguzi wa halmashauri ya manispaa ya Tabora Elias Kayandabila amemtangaza mgombea wa chama cha mapinduzi Ndulila Pandauyaga kuwa mshindi wa nafasi ya udiwani katika kata ya Ndevelwa.

Wakati anatangaza matokeo hayo ameweka wazi namna uchaguzi ulivyokuwa pamoja na matokeo yake.

Amesema kuwa Ndulila ameongoza Kwa kura 2608 sawa na asilimia 97 ambapo aliemfuata ana jumla ya kura 21.

Aidha amebainisha kuwa Kwa idadi ya kura hizo bwana Ndulila amekua diwani wa kata ya Ndevelwa hiyo rasmi.

Kata ya Ndevelwa halmashauri ya manispaa ya Tabora ni moja kati ya kata nchini iliyofanya uchaguzi mdogo.

Mwisho. 

Post a Comment

Previous Post Next Post