Na Jumbe Ismaily
WAKULIMA wa tumbaku katika vyama vitano vya ushirika vya msingi vilivyopo kata ya Mitundu,Halmashauri ya Itigi,wilayani Manyoni katika msimu uliopita wa kilimo walizalisha jumla ya kilo 736,988 zenye thamani ya dola za kimarekani 1,809,382.20.
Akitoa taarifa fupi ya ununuzi wa tumbaku wakati wa hafla fupi ya kukabidhi madawati 55 kwa ajili ya shule za msingi na milango minne ya kituo cha polisi Mitundu,Meneja uhusiano na Usimamizi wa Kampuni ya tumbaku,Yusufu Mahundi aliweka bayana kwamba kwa mwaka mmoja wamenunua zao hilo na hivi sasa wanaingia mwaka wa pili kununua tumbaku katika wilaya ya Manyoni,hususani katika eneo la Mitundu.
katika Halmashauri nane za mikoa mitano inazofanyaka kazi hapa Nchini ambapo huchangia madawati,visima vya maji,vifaa vya Hospitali,vifaa vya ujenzi pamoja na vifaa vya michezo vyenye jumla ya shilingi milioni 162,832,737.


Post a Comment