Na Amini Nyaungo
Wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi wametakiwa kufuata katiba na
utaratibu ili uchaguzi ufanyike kwa haki na weledi wa hali ya juu.
Hayo ameyasema leo Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Singida
Mjini Aminiel Mfinanga alipokuwa mgeni rasmi katika ufugnuzi wa mafunzo ya siku
tatu ya wasimamizi wa uchaguzi ngazi ya Kata katika Manispaa ya Singida.
“ Najua mafunzo haya yatawaweka vizuri kuwakumbusha utaratibu wa
uchaguzi , ili uchaguzi uwe mzuri lazima mtende haki kwa washiriki wa vyama
vyote,”Mfinanga
Katika hatua nyingine amesema kuwa uchaguzi ni mchakato
unaojumuisha hatua na tarabu za katiba na sheria ambazo zinatakiwa kufuatwa,
amewataka kuondoa malalamiko na vurugu wakati wote wa uchaguzi.
Aidha kwa upande wa Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Mwanzo Utemini
Mkoani Singida Ferdinandi Njau amewashauri wanaopata mafunzo kufuata sheria.
“Katika mambo ya kuzingatia walichoapa wanakizingatia ili
uchaguzi uwe huru na haki,” Njau
Lakini pia Afisa uchaguzi jimbo la Singida Mjini Beno Magessa
amesema namna semina hiyo itawasaidia kuwakumbusha maswala ya uchaguzi ambapo
kutakuwa na mada 11 zitakazo jadiliwa.
“ Jumla ya mada 11 zitajadiliwa kwa siku tatu tunatemea baada ya
hapa watakuwa wameelewa na tunategemea uchaguzi utakuwa wa haki na huru,”BENO
Kwa upande wa wasimamizi Wasaidizi nao wamesema kuwa mafunzo
hayo yatawanufisha katika kutenda haki.
Mwisho
Post a Comment