WAJUMBE WASEMA ‘YES’ KWA KISHOA IRAMBA MASHARIKI



Na Amini Nyaungo



Wajumbe wa Jimbo la Iramba Mashariki wameamua kumchagua aliyekuwa Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Singida mzaliwa wa Mkalama kata ya Nduguti Jesca David Kishoa baada ya kumpitisha katika kura za maoni kwa kura za kishindo siku ya jana August 04,2025 kwa kumpa kura 5946.



Hii ni baada ya kurudishwa majina saba (7) ya wagombea ambao walijinadi kwa sera zao na hatimaye Kishoa kuibuka mshindi kati ya hao.

Kishoa amemshinda aliyekuwa Mbunge wa Jimbo hilo Francis Isack aliyepata kura  kura 2932 za wajumbe ambazo hazikutosha kumrudisha katika kinyang’anyiro.

Kupata kura za ndio kwa Kishoa kuna ashiria yale mazuri aliyoyafanya wakati akiwa Mbunge wa Viti Maalum kwa kuwa karibu na wananchi pamoja na kuwasikiliza katika adha zao za kawaida zikijumuisha zile za binafsi pamoja na za ujumla.



Baada ya ushindi huo Kinachosalia sasa ni kurudishwa jina lake CCM Taifa baada ya mchakato basi sasa apeperushe bendera ya Chama Cha Mapinduzi(CCM) katika Jimbo hilo.

Wengine waliotia nia ni pamoja na Amani Mwendoss aliyepata kura 76, Amam Kwale kura 216, Ally Hassan Ilanga kura 526, Allan Joseph Kiula kura 446 na Joel Kingu Misholi kura 316.

Mwisho.

 

Post a Comment

Previous Post Next Post