TANZANIA KUJITEGEMEA MIAKA 25 YA DIRA YA TAIFA YA MAENDELEO

Na Amini Nyaungo



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dokta Samia Suluhu Hassan amesema kuwa Tanzania imejaliwa maliasili ambazo zinaweza kuwa chachu ya maendeleo ya nchi zikiendelea kutumika vizuri.

Ameyasema hayo leo Julai 18,2025 katika uzinduzi wa Dira ya Maendeleo ya Taifa ya mwaka 2025-2050 mkoani Dodoma.

Katika Hotuba yake Rais Dokta Samia ameweka wazi kuwa dira imekusudia mambo mengi sana moja wapo ni kutumia rasilimali za nchi ili kuweka kujiendeleza kiuchumi na KUJITEGEMEA.

Rais Dokta Samia amesema kuwa Misaada na mikopo ikitumika vizuri inaweza kusaidia maendeleo ya nchi lakini kipaumbele namba moja katika dira ambayo ameizindua leo ni kutumia rasilimali  zilizopo na kujitegemea.

“Misaada na mikopo ikitumika vizuri inaweza kusaidia maendeleo ya nchi kipaumbele chetu ni kutumia rasilimali zetu  zilizopo ili kuendeleza nchi yetu kwa hiyo lengo kuu ni kujitegemea,” Rais Dokta Samia.

“Lazima Tanzania iwe sehemu ya kutumia mabadiliko ya akili mnemba kwendana na dunia ya leo”



Aidha katika hotuba yake pia ameweza kugusia kuwa ili dira iweze kutumika kama ilivyokusudiwa lazima Watanzania wote wawe  wamoja  kulikweka taifa katika maendeleo, akisema kuwa Serikali,Sekta Binafsi wafanyekazi zaidi kuliko maneno.

“Tumejiwekea lengo la kuweka taifa Jumuishi lenye haki na maendeleo, katika dira ya 2050 tutende sana kuliko kusema, Serikali, Sekta binafsi tutende zaidi kuliko kusema,”amesema

Katika sehemu ambazo pia Rais Dokta Samia amegusia ni pamoja na kutokana na kukua kiuchumi na kuibuka kwa mataifa mbalimbali kukua kiuchumi taifa la Tanzania katika sera na diplomasia ya kimataifa itaendelea na sera yake ya kutofungamana nan chi yoyote.



“Tanzania kuendelea na sera yake ya kutofungamana na nchi yoyote,”

Aidha pia ameelekeza tume ya taifa ya Mipango waandae haraka nyenzo zitakazo tumika kupima kipimo cha maendeleo serikalini.



“ Naelekeza kila wizara kupitia sera zake zile ambazo haziendani na dira hii basi waziache, Tume ya kurekebisha sharia Tanzania waanze mchakato wa kuchambua juu ya dira hiyo,Kuelekeza dira ya mipango kuweka mfumo wa muda wa utekelezaji wa hatua kwa hatua, Sekta binafsi inatakiwa kujipanga ili itekeleze malengo na shabaha ya dira hiyo,” ameongeza

Mwisho 

Post a Comment

Previous Post Next Post