REHEMA SOMBI AJITOSA KUWANIA UBUNGE VITI MAALUMU KUPITIA VIJANA

 Na Robert Onesmo



Makamu Mwenyekiti wa umoja wa vijana(UVCCM) taifa Rehema Omary Sombi ,amechukua na kurejesha fomu ya kuomba ridhaa ya kugombea Ubunge wa viti maalumu  katika uwakilishi wa kundi la vijana taifa



Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kurejesha fomu hiyo Rehema, amesema anaipongeza sekretarieti ya Chama Cha Mapinduzi kupitia kwa katibu mkuu wake  Dkt .Emmanuel Nchimbi kwa namna alivyoratibu zoezi hili ambalo limeenda kwa amani na utulivu



Kwa upande wake Sombi amejitanabaisha kuwa ameshakwisha kuiva katika eneo la utekelezaji wa irani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)



"Niwahakikishie heshima ambayo niliipata nimeshakwisha kukwiva lakini sisi kama chama cha Mapinduzi ni wamiliki wa duka sasa tunaenda kule ili tukatunge sheria ambazo zitawalinda vijana ambapo sisi ndio tunaomba dhamana kwa upande huo"amesema Sombi.



Post a Comment

Previous Post Next Post