.
Na Mwandishi Wetu
Jeshi
la Polisi Tanzania limetoa taarifaa ya matukio mbalimbali yalitokea moja ya taarifa
hiyo ni kutoka mkoani Singida ambapo Sheikh ZUBERI NKOKOO kutoonekana taarifa Zaidi
ya tukio hilo inasema kuwa ametengeneza ionekane ametekwa kwakuwa alikuwa
anadiiwa madeni.
KWA
TAARIFA ZAIDI HII HAPA KUTOKA JESHI LA POLISI MAKAO MAKUU DODOMA
Miongoni
mwa matukio hayo ambayo yamethibitishwa kwa sababu hizo ni pamoja na tukio la
hivi karibuni lililomhusisha Shekhe Zuberi Said Nkokoo (53) mwalimu wa dini na
kiongozi katika taasisi ya Islam Foundation iliyopo mkoani Singida ambayo pia
inajishughulisha na Miongoni mwa matukio hayo ambayo yamethibitishwa kwa sababu
hizo ni pamoja na tukio la hivi karibuni lililomhusisha Shekhe Zuberi Said
Nkokoo (53) mwalimu wa dini na kiongozi katika taasisi ya Islam Foundation
iliyopo mkoani Singida ambayo pia inajishughulisha na Anwani ya Simu: “MKUU
POLISI” Simu Namba: 026 2323585 Fax: 026 2323586 E – Mail: info.phq@tpf.go.tz
Ofisi ya Mkuu wa Jeshi la Polisi, Makao Makuu ya Polisi, 4 Mtaa wa Posta, S. L.
P. 961, 40483 DODOMA 2 shughuli za kuchinja wanyama.
Katika
tukio hilo kupitia vyombo mbalimbali vya habari ikiwemo mitandao ya kijamii
kulisambaa taarifa za kutekwa kwa Shekhe huyo na watu aliowataja kuwa ni askari
wa Jeshi la Polisi tarehe 02/06/2025 saa tano usiku akiwa na kiasi cha fedha
taslimu shilingi za kitanzania milioni arobaini na mbili (Tshs.
42,000,000/=).Taarifa ya kupotea kwake pia iliripotiwa Polisi.
Baada
ya uchunguzi, ilibainika kuwa Shekhe Zuberi Said Nkokoo hakuwa ametekwa bali
alitengeneza tukio la uongo la kutekwa ili kukimbia madeni aliyokuwa akidaiwa
na watumbalimbali (majina yao yamehifadhiwa) yenye jumla ya shilingi za
kitanzania milioni mia tano ishirini na moja na laki tano (Tshs.
521,500,000/=). Shekhe Zuberi atafikishwa Mahakamani baada ya taratibu za
kisheria kukamilika.
KUHUSU
KUPOTEA AU KUTOONEKANA KWA WATU MBALIMBALI NCHINI
Kumekuwepo
na kuripotiwa kwa taarifa katika vituo vya Polisi na nyingine katika mitandao
ya
kijamii zikijulisha kwamba mtu au watu fulani wamepotea, hawaonekani au
wamekamatwa
na watu waliojitambulisha kuwa askari wa Jeshi la Polisi.
Jeshi
la Polisi linapopokea taarifa hizo, huanza uchunguzi kwa kukusanya ushahidi
kutoka
vyanzo
mbalimbali ili kupata ukweli wa taarifa ya nini kilichotokea kwani hauwezi
kusema
moja
kwa moja kuwa mtu aliyeripotiwa kupotea, kutekwa, kulazimishwa kupotea au
kuuawa
bila ya kumpata anayedaiwa kupotea na ushahidi wa kuthibitisha taarifa hiyo ya
nini
kilichomtokea, kama alitendewa uhalifu ni nani wahusika, kulingana na sheria,
kanuni
na
taratibu.
Vilevile,
kwa mujibu wa kifungu cha 117 cha Sheria ya Ushahidi Sura ya 6 marejeo ya
mwaka
2022 na kifungu cha 161 cha Sheria ya Ndoa Sura ya 29 marejeo ya mwaka 2019,
dhana
ya mtu kuchukuliwa kuwa amekufa inapaswa kuthibitishwa na mahakama baada ya
miaka
mitano kupita kulingana na vielelezo na ushahidi utakaowasilishwa.
Katika
matukio ambayo yameripotiwa katika vituo vya Polisi na uchunguzi wa kina
kufanyika
na walioripotiwa kupotea kupatikana wakiwa hai na wengine wakiwa wamekufa,
hadi
sasa ushahidi kwa baadhi ya matukio yameonesha sababu zake ni kujiteka, wivu wa
mapenzi,
imani za kishirikina, kugombea mali, kulipiza kisasi, kwenda nchi nyingine
kujifunza
misimamo mikali na kukimbia mkono wa sheria baada ya kufanya uhalifu
Post a Comment