Na Amini Nyaungo
Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania DKT. Samia Suluhu Hassani ameitendea haki miradi yote
iliyoanzishwa na mtangulizi wake hayati DKT John Joseph Magufuli hivyo anastahili kuwa katika kiti hicho kwa awamu nyingine ili
amalize yale yaliyobaki.
Hayo ameyasema leo Kada
wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Singida Japhari Saidi alipoongea na
Waandishi wa Habari leo (Juni 8,2025) katika ukumbi wa Rafiki Mkoani hapa.
Aidha katika mkutano huo
ameweka wazi kuwa pasipo na mashaka Rais DKT. Samia ameendeleza pale ambapo
mtangulizi wake amepaachaa kwani ameweza kuitendea haki miradi mikubwa ya
maendeleo.
“ Rais DKT. Samia
ameitendea haki miradi yote iliyoanzishwa na mtangulizi wake,” amesema
Japhari ameweka bayana
kuwa anayoyafanya hivi sasa Rais Dokta Samia
Suluhu Hassan ni kielelezo cha ukomavu na uzalendo katika aifa hili la
Tanzania.
“Anayoyafanya Rais DKt
Samia ni kielelezo cha ukomavu na uzalendo wake kwa Taifa la Tanzania,” Japhari
Kada huyo ameenda mbali Zaidi
na kusema kuwa kwa yote aliyoyafanya anastahili kuwa katika nafasi aliyyopo
hivi sasa kwani ameimudu vizuri.
“ Rais DKt Samia amethibitisha
pasipo shaka yeyote kuwa anatosha kwa nafasi hiyo,” Ameongeza
Licha ya hayo amesema
kuwa kila idara hivi sasa iko katika wakati mzuri kwani katika uongozi wake
ameweza kuimarisha utu na usawa kuanzia katika afya, michezo hadi Sanaa huku
akiwa kinara katika kuweka sawa miundombinu.
“Kwa wakati huu kila kitu
kipo vizuri ukiangalia katika michezo viwanja vizuri vipo kwa ajili ya kuchezo
michuano mikubwa ya kimataifa na kitaifa kwenye afya nako amefanya vizuri kwani
kuna zahanati kila sehemu pamoja na miundombinu bora,”
Mwisho
Post a Comment