HISTORIA YA MANISPAA YA SINGIDA KIARATU AIPENDEZESHA

Na Amini Nyaungo



Singida moja ya mikoa ambayo imechangamka katika kila nyanja, upande wa michezo uko sawa, upande wa vyombo vya habari nayo inafanya vyema katika kuutangaza Mkoa wa Singida kila mmoja anafanya katika upande wake.

Upande wa siasa pia unaendelea kufanya vizuri mno Singida imetoa Waziri wa Fedha ambaye ni Mwigulu Lameck Nchemba ina viongozi wakubwa ambao wanaiwakilisha vyema Singida.

Makala yangu inaangaziaa zaidi Manispaa ya Singida ambapo ina historia nzuri mno ila leo nitaangalia historia ndogo sana ya Manispaa hii ilipoanzia hadi kufikia leo na huko mbele utaona dhamira ya kichwa cha habari hapo juu.

Kabla ya kuwa Manispaa ya Singida hapo zamani iliitwa Halmashauri ya Mji wa Singida wakati harakati za kumegwa kati ya Singida Mjini na Singida Vijijini ilipatwa kuitwa Wilaya Ndogo na miongoni mwa Wakurugenzi wa mwanzoni kabisa walikuwa ndugu Lipendele pamoja na mama yetu mama Sumari.

Hata hivyo Wilaya ndogo hiyo haikupewa Mkuu wa Wilaya bali Mkuu wa Wilaya ya Singida aliendelea kutawala Wilaya zote mbili hali ambayo imeendelea hadi hivi sasa.

Kiini cha Makala hii huko kote nimekupa historia lengo langu ni kuangazia viongozi ambao waliwahi kuongoza  kuanzia Halmashauri ya Mji wa Singida hadi kuitwa Manispaa ya Singida na hapa tunaanzia  mwaka 1981 katika eneo la uongozi ambapo zamani waliitwa Wenyeviti wa Mji wa Singida kwa sasa wanaitwa Meya.

Ni miaka 20 sasa imepita tangu ibadilishwe na kuitwa Manispaa ya Singida na hapo sasa pia imebadilika viongozi wake waliitwa MEYA yaani Meya wa Manispaa ya Singida.

Tukianzia hapo Yagi Maulid Kiaratu ambaye sasa anagombania Ubunge wa Jimbo la Singida Mjini akiongoza katika kura za maoni za wajumbe ila kabla ya hapo alikuwa  Mstahiki Meya wa Manispaa ambapo  anakuwa ni wa tatu baada ya wawili kutangulia kuongoza Manispaa hii( Yaani hao wawili na ukijumisha Mheshimia Yagi wanakuwa wa tatu  na ukijumlisha na wale wenyeviti wanakuwa 8).

Wameanza kuitwa Meya wa Manispaa ya Singida mwaka 2005 hadi sasa ni miaka 20 imepita na mji wa Singida unaendelea kuwa katika mazingira mazuri.

Wakwanza kabisa kuzindua kuwa Meya wa Manispaa ya Singida ni ndugu yetu Mheshimiwa Salum Mahami yeye amekaa hapo kwa miaka kumi kuanzia 2005 hadi 2015.

Mwaka 2015 hadi 2020 amechukua mzee wetu Mheshimiwa Gwae C. Mbua  kwa miaka mitano ambayo amehudumu kama Meya wa Manispaa ya Singida.



Wakati huo Gwae anachukua jukumu la kuwa Meya moja ya wasaidizi wake katika hiyo miaka 5 aliyohudumu  Mheshimiwa Yagi Kiaratu aliwahi kuwa Naibu Meya na kufanyanae kazi vyema sana.

Ngoma imebadilika kutoka kuwa Naibu Meya ambapo mwaka 2020 hadi 2025 Mheshimiwa Mstahiki Meya Yagi Kiaratu amekuwa akiongoza kiti hiko kwa uzuri sana na roho safi sana.



Hivi sasa Gwae Mbua ndio Naibu Mstahiki Meya kibao kimegeuka na historia imeandikwa kwa wino mweusi kwa kukolezwa.

Yagi amekuwa akifanya mzuri na kuipendezesha  Manispaa ya Singida na ni mmoja ya viongozi wenye mvuto wa hali ya juu sana.

Mji wa Singida unakua na unaendelea kupendeza hivi sasa yote haya ni usimamizi mzuri wa viongozi wa mkoa wa Singida pamojana Mstahiki Meya Yagi Kiaratu.

Kwanini mama huyu asiandikwe katika wino mweusi na kukolezwa kwa jitihada anazozifanya ? ni jembe sana huyu mama wala sio masikhara, ana utu na utulivu pamoja na kujali watu wake.

Pia ni diwani  wa kata ya Majengo hebu kaangalie katika Kata hiyo namna ambavyo imejengeka na ilivyosafi kazi yake imeendelea kuonekana.

Ukiachana na hapo orodha ya MEYA tangu iiliyobadilika mwaka 2005 ifuatayo ni orodha  ya Wenyeviti wa Mji wa Singia rasmi ilianzia mwaka 1981 ambapo Mathayo J. Hango ameongoza kiti hiki kwa mwaka mmoja mmoja hadi mwaka 1982.

Safari iliendelea ambapo Rajabu W. Munkhola amechukua nafasi hiyo mwaka 1983 hadi Disemba 1983 akaachia ngazi na kuwapa kijiti wengine.

Mwaka 1984 hadi 1988 alikuja ndugu Hassan T. Simba yeye amekaa kwa miaka mine katika cheo hicho ambacho kwa sasa ndio kama Meya wakati huo kinaitwa Mwenyekiti wa Mji wa Singida.

Baada ya hapo akachukua nafasi Hassani Simba Ikuja kutokea mwaka 1989 hadi 1998 yeye amekaa kwa miaka 9 katika kiti hicho na kumuachia mwingine.

Katika orodha hiyo wa mwisho alikuwa Salum M. Mahami yeye sasa akaongoza kuanzia 1998 hadi mwaka 2005 amekaa kwa miaka 7.



Baada ya hapo ndio ikabadilika ikawa Manispaa ya Singida ambayo tayari nimeielezea juu kuanzia mwaka 2005 hadi sasa 2025 inatambulika kama Manispaa ya Singida na wanaoongoza ni Meya sio Mwenyekiti tena wa mji wa Singida.

Kwa ujumla wake ni viongozi 8 ambao kila mmoja ametoa huduma yake kwa vile ambavyo Mungu alivyomjalia na kuiongoza Singida katika njia salama.

Manispaa ya Singida ndio ina kila kitu  ina soko kuu la Mkoa wa Singida, ina Soko la Vitunguu, ina soko la Matunda ina Stand Kuu ya Mabasi pamoja na mambo mengine mazuri ambayo yanaipeperusha Singida.


Kwa sasa Mheshimiwa Yagi Kiaratu amepita katika kura za maoni na anasubiri kamati kuu itasemaje juu ya kupeperusha bendela ya Ubunge Jimbo la Singida Mjini.


Yagi kwa Mujibu wa watu mbalimbali anapendwa sana na watu hasa katika kujitoa kwake kwa mtu mmoja mmoja na kundi la watu na Wanasingida kwa ujumla.

Singida ni sehemu salama yoyote aitakaye aje.

Mwisho 

Post a Comment

Previous Post Next Post