WAKULIMA WAAMBIWA WASILETE VITUNGUU SOKO KUU KWA SIKU MBILI

Na Amini Nyaungo


Wakulima na Wafanyabiashara wa bidhaa ya Vitunguu mkoani Singida wameombwa kutopakia bidhaa hiyo kutoka mashambani kwa muda wa siku mbili kutokana na kujaa  katika soko kuu la vitunguu mkoani hapa na endapo watapakia itasababishwa kukaa bila kushushwa wanapofika sokoni  kwakuwa  hakuna sehemu ya kushusha.

Hayo ameyazungunza leo (March,20,2025)  Mwenyekiti wa Soko Kuu la Vitunguu mkoani Singida Iddi Mwanja alipozungunza na Chamber Media alipotembelea sokoni akiwaambia wananchi na wakulima kuwa leo bidhaa imefurika sokoni hivyo zikiendelea kupakiwa huko mashambani watakosa sehemu ya kushushwa na kusababisha usumbufu kwa mkulima.


“Leo vitunguu vimejaa hakuna sehemu ya kuweka hivyo nawaomba radhi wakulima waliopo mashambani wanataka kupakia mazao yao watulie kwa siku mbili ili huu mzigo uliopo uishe au upungue ili waweze kuingiza vitunguu vingine,” Mwanja

Aidha amejibu juu ya baadhi ya wafanyabiashara wanaotaka waongeze ujazo ili wanunue Vitunguu hivyo kwa haraka ameweka bayana kuwa ujazo utabakia kuwa kama ilivyo kawaida gunia moja ujazo wake ni kilo100 hadi 105 wala hawajazi ‘Shishimbi’ ili kwenda sawa misimamo waliojiwekea na kama ambavyo serikali inahitaji.

“Nimesikia kwa wafanyabiashara wanataka ujazo uongozeke hapana hapa tunajaza kama ilivyo kawaida hatuongezi ujazo, Serikali inataka hivyo hata sisi tumeweka utaratibu huo hakuna kuongeza kipimo ili mkulima asipunjwe,”

Kwa upande wao wakulima ambao ndio wafanyabiashara wa zao hili wameweka wazi kuwa uongozi usimimashe kuingiza biashara hiyo kwa siku chache ili mzigo uliopo uishe lakini pia wengine wakitaka waongeze ujazo ili mzigo wao ukamilike.

Kwa upande wake Mbuga Rashidi yeye ni mkulima ameshauri uongozi uongeze ujazo huenda  ikawa njia sahihi ili mazao yao yauzwe haraka

“Mie naona waongeze kidogo ujazo ndio inakuwa njia rahisi ya mazao yetu kuuzwa haraka vinginevyo tutakesha hapa,” Mbuga

Akiungwa mkono na Yahya Mohamed ambaye pia amesema waongeze ujazo ili kila kitu kiende sawa na mzigo uliopo uishe na wanedelee na shughuli nyingine.

Lakini Omari Shabani yeye amesema kuwa ni veyma uongozi wawaambie wananchi na wakulima wasilete mazao yao kwanza hadi mzzigo huu utakapo isha.

“Kwa hapa ili siku ya leo gunia limesimama hata elfu sabini ambapo juzi tu ilikuwa hadi laki a thelethini leo mzigo upo wa kutosha hapa hivyo uongozi uone namna ya kuwaambia wakulima wasilete mazao yao,” 

Post a Comment

Previous Post Next Post