Na Jumbe Ismailly MANYONI
SERIKALI kupitia Wakala wa Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania
(TAWA) Kanda ya kati imefanikiwa kuingiza takribani shilingi bilioni
12,657,626,387.60 kutokana na shughuli za utalii zinazofanyika katika mapori ya
Akiba ya Rungwa-Kizigo na Muhesi.
Kamanda wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania
(TAWA) Kanda ya kati,Kamishna Msaidizi Mwandamizi,Herman Nyanda amebainisha
hayo alipokuwa akielezea faida zitokanazo na utalii na kwamba kiasi hicho cha
fedha kimepatikana katika kipindi cha mwaka wa fedha wa 2022/2023,2023/2024 na
2024/2025.
Aidha Kamanda huyo wa Tawa Kanda ya kati amefafanua kuwa
utalii wa uwindaji unahusisha seehemu kubwa ya kanda ya kati-Manyoni Mkoani
Singida na unafanyika katika Mapori ya Akiba matatu ambayo ni pamoja na
Rungwa,Kizigo na Muhesi na eneo la nje la Rungwa-North lililopo Halmashauri ya
Itigi.
Kwa mujibu wa Kamishna Nyanda mapori hayo kwa pamoja yana
jumla ya vitalu 12 ambapo pori la Akiba Rungwa lina vitalu sita,Kizigo vitalu
vinne,Muhesi kitalu kimoja na Rungwa North Open Area kitalu kimoja na kwamba
kati ya vitalu 12 vilivyopo,vitalu tisa vimepata wawekezaji wa utalii wa uwindaji.
Akifafanua zaidi kamishina huyo amesema wawekezaji hao
wamekuwa wakifanya kazi za uhifadhi,kuboresha na kujenga miundombinu ya
kitalii, kufanya shughuli za kitalii na kupitia uwekezaji huo,serikali imekuwa
ikipata mapato mbali mbali yanayojumuisha ada za vitalu,tozo za wanyama
wanaowindwa,malipo ya vibali vya uwindaji wa kitalii na malipo ya watalii
wasindikizaji.
Ameweka bayana kwamba Tawa kanda ya kati pia inasimamia
vitalu vya uwindaji wa kitalii vilivyopo kwenye maeneo ya wazi vya Rungwa
kaskazini pamoja na Rungwa kusini ambapo katika kipindi cha miaka mitatu ya
2022/2023 hadi 2024/2025 serikali kupitia Tawa Kanda ya kati imeingiza
takribani shilingi bilioni 12,657,626,387.60 kupitia shughuli za utalii
zinazofanyika katika mapori ya Akiba Rungwa Kizigo na Muhesi.
Akizungumzia wanyamapori,wakali na waharibifu,Kamanda huyo wa
Tawa Kanda ya kati hata ameweka bayana kuwa kanda ya kati inakabiliwa na
changamoto kubwa ya uwepo wa matukio ya wanyamapori wakali na waharibifu katika
maeneo ya wilaya mbali mbali za Mkoa wa Singida.
Ameyata maeneo mengine yenye changamoto kuwa ni pamoja na
wilaya ya Manyoni,Ikungi,Mkalama,Singida vijijini,Singida mjini pamoja na
wilaya ya Iramba na kwamba kazi za kudhibiti wanyamapori wakali,waharibifu
kwenye maeneo mbali mbali ya vijiji vilivyopo katika wilaya hizo,imeweza kuokoa
maisha ya wananchi na mali zao kama vile mazao,mifugo,makazi na uwindaji haramu
wa wanyamapori.
Katika kuhakikisha usalama wa wananchi na mali zao,Kamishina
Nyanda amesema ofisi ya Kanda pamoja na Mapori ya Akiba kwa kushirikiana na
Halmashauri za wilaya husika wamekuwa wakifanya doria za kuzuia wanyamapori
wakali na waharibifu kwa kushirikiana na
askari wa akiba wa vijiji katika wilaya husika
MWISHO.

.jpg)
Post a Comment