NHIF SINGIDA WATOA VIFAA VYA KUJIFUNGULIA KINA MAMA MKALAMA

 

Na Amini Nyaungo



Jamii imehimizwa kujiunga na mfuko wa Bima ya Afya Taifa (NHIF) ili iwasaidie pale wanapopatwa na magonjwa mbalimbali watibiwe kwani magonjwa yanakuja bila ya taarifa hivyo wakiwa na bima wanakuwa tayari kwa ajili ya kupata matibabu.



Hayo ameyasema leo Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoa wa Singida Benjamini Mwalugaja Wilayani Mkalama ambapo walikuwa wanagawa mifuko hiyo ambayo ndani yake kumesheheni vifaa kwa ajili ya kina mama kujifungulia yaani ‘’Delivery park’’.

Mwalugaja amesema kuwa hiyo ni zawadi kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya DR. Irine  Isaka kwa ajili ya wanawake kusaidia kupata vifaa vya kujifungulia akisema kuwa hayo ni maono ya Rais Daktari Samia Suluhu Hassan katika kutoa huduma bora kwa wananchi wake.



“ Leo tumetembelea Wilaya ya Mkalama ikiwa ni muendelezo wa siku ya mwanamke Mkurugenzi wetu wa mfuko wa Bima ya Afya ya Taifa dokta  Irene Isaka ameitoa kwa ajili ya wanawake vifaa vya kujifungulia haya pia ni maono ya Rais Daktari Samia kwa kina mama,”

Mganga mfawidhi wa Kituo cha Afya cha Kinyangiri ANNA PETER amesema kuwa vifaa hivyo ni muhimu kwa wanawake wanapofikia wakati wa kujifunga huku akimpongeza Rais Dokta Samia kwa jitihada zake kwa wananchi wake.

“ Hivi vifaa vitasaidia sana kwa wanawake hawa ambao wanaelekea kujifungua lakini pia NHIF nao tunawashukuru kwa kusambaza vifaa hivi,” DK. ANNA



Kwa Upande wake Dokta Nikasi Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Wilaya ya Mkalama amesema kuwa vifaa wamevigawa kwa watu wanaostahili akiwashukuru Bima ya Afya Singida kwa kazi nzuri wanayoendelea kuzitoa kwani wao kama watoa huduma zitasidia kutoa huduma bora.

Nao wanufaika wa vifaa hivyo Ester Samwel na  Rechal Misana ambao ni mama wajawazito wamesema kuwa vifaa hivyo  vitasaidia kupata uzazi salama huku wakishukuru NHIF kwa jitihada zao za kuzisambaza.



Naye Afisa wa wanachama NHIF Mkoa wa  Singida Tatu Yassin  amehimiza wa mama wawakatie bima za afya ili wasije wakapata taabu wanapofikia wakati wa kujifungua na kuwaomba kujiunga na NHIF.

“Ni waombe watu wajiunge na NHIF kwani ni muhimu mno kwa ajili ya maisha yao niwaambie hii ni salama kwao waje  wajiunge wakate bima,” Tatu

Katika msafara huo wametembelea Kituo cha Afya cha Kinyangiri pamoa na Hospitali ya Halmshauri ya Mkalama.

Post a Comment

Previous Post Next Post