GWAU ATISHA IKUNGI, UWT WAMPONGEZA, LIKAPAKAPA ATIA NENO

Na Amini Nyaungo

Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Singida Martha Gwau amewataka Umoja wa Wanawake Wilaya ya Ikungi (UWT) kuchangamkia fursa ya mikopo ya asilimia kumi inayotolewa na Serikali inayoongozwa na Rais Daktari Samia Suluhu Hassan ili waweze kujikomboa kiuchumi na familia zao.
Ameyasema hayo leo (February 9,2025) katika Semina iliyofanyika Wilaya ya Ikungi ikiwalenga Umoja wa Wanawake Wilayani hapa na kuwashauri wasisite katika kuchkua mikopo kwani itawasaidia katika maendeleo ya maisha yao.
“Baada ya kupata fursa ya elimu iliyotolewa na Wataalamu juu ya mikopo naomba msisite kuchukua mikopo itawasaidia katika kuleta maendeleo ambapo Rais Dokta Samia ameweza kuwajali kwa kuwapa mikopo isiyo nariba,”Gwau

Semina hiyo  ameigharamia na kuhusisha kada mbalimbali za wataalam wakiwemo Maafisa Maendeleo, Watu wa Benki, Watu wanaohusika na mbolea pamoja na watu wa Mbegu akiwa na lengo la kuwapa elimu kina mama katika Nyanja mbalimbali za maendelo.

Katika hatua nyingine Gwau amempongeza Rais Dokta Samia Suluhu Hassan kwa kazi nzuri anayoendelea kuifanya katika jamii ya Kitanzania.

“Rais Samia anaendelea kutuonyesha namna gani anaupendo kwa wananchi hasa katika kuleta fursa na miradi ya maendeleo naomba tuendelee kumuunga mkono,” Gwau
Katika semina hiyo alihudhuria Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Ikungi Mika Tano Likapakapa amempongeza Mbunge huyo kwa kazi nzuri anayoifanya.

Mwisho..

Post a Comment

Previous Post Next Post