KISHOA AYASEMA MAZURI YA RAIS SAMIA BUNGENI

 

Na Amini Nyaungo
Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Singida, Jesca Kishoa, amempongeza Rais  wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Daktari Samia Suluhu Hassan bungeni Dodoma leo( Januari 31, 2025) wakati wa kuchangia hoja mbalimbali ambapo  katika mchango wake, Kishoa alisisitiza maono makubwa ya Rais katika sekta ya nishati na maendeleo ya nchini.
Kishao amesema kuwa Tanzania imejaliwa kuwa na Rais mvumilivu na mwenye uwezo wa kuimarisha demokrasia na diplomasia ya uchumi pia alihimiza umuhimu wa kuhakikisha maendeleo yanapatikana katika Wilaya ya Mkalama.
Katika hatua nyingine amewaomba Watanzania kuhakikisha amani inaendelea kulindwa akitoa mifano ya nchi ambazo hazina amani wanaotesa watoto, Wazee na kina mama.

"Tulinde amani tuliyonayo watu wa usalama wasicheke na mtu anayetaka kuharibu amani ya nchi yetu wanaoumia Wazee, Watoto na wanawake,"Kishoa
Pamoja na yote Kishoa amewaunga mkono wajumbe wa CCM walioketi katika mkutano mkuu ambao wamekubaliana kumchagua Rais Daktari Samia Suluhu Hassan kuwania nafasi ya Urais katika uchaguzi mkuu utakao tarajiwa kufanyija Oktoba mwaka huu.

 Mwisho 

Post a Comment

Previous Post Next Post