HABARI

MICHEZO

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

HABARI

HABARI

MAKALA

» » WASHIRIKI MAONYESHO YA UWEZESHAJI SINGIDA WAFURAHI WADAU WAFIKA

 

Na Amini Nyaungo

Maonyesho ya saba ya Uwezeshaji yanaendelea mkoani Singida ikiwa kesho Jumamosi ndio tamati ya maonyesho hayo Naibu Waziri Mkuu Dokta Dotto Bitteko atakuwa mgeni rasmi, wadau na washiriki wafurahishwa na maonyesho hayo.

Chamber Media imetembelea washiriki ambao ni Taasisi na Kampuni mbalimbali kwa ujumla wake wafurahishwa na maonyesho huku walio wengi wamepata kile walichofuata.


Aurelia Masasi yeye ni Afisa Uwekezaji wa EFTA amesema wamekuja mkoani Singida kuonesha bidhaa walizokuja nazo ikiwemo "Power Tila" naTrekta ambazo wanakopesha na kupitia maonyesho hayo watu wawili wameshanunua bidhaa yao.

"Tumefurahishaa na hizi tunaendelea kuwaita wadau na watu mbalimbali kutembelea banda letu ili wajionee na wakipendezwa wachukue bidhaa zetu," Aurelia.

Naye Amina Hassani Mkurugeni wa Kampuni ya bidhaa za nyuki "Mwangaza Honey Food Company" ametokea mkoani Tabora.

Yeye amewakaribisha wadau lakini pia amewataka wafike bandani kwao ili wapate kuona bidhaa nzuri kutoka kwao.
Naye Victoria Emanuel wanajihusisha na madawa ya mifugo ambapo wametumia fursa hiyo kuitangaza biashara kwa kuwa ndio wanaanza.

Manji Jackson kutoka NHIF wao wapo hapo akisema mahudhurio mazuri sana banadani kwao na wanaendelea kuhimiza watu kujiunga na mifuko ya hifadhi ya Jamii.

Mwisho

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply