Charles Kikiricho
Wananchi wameombwa kujitokeza katika vituo vya afya kwaajili ya kupima ugonjwa wa kifua kikuu ili waweze kupata tiba kwani ugonjwa huo unatibika.
Wito huo umetolewa na Daktari wa kifua kikuu Isabela Nyamizi wakati akiongea na Standard Radio asubuhi ya leo 18/09/2024 ya kuwaomba wananchi wajitokeze ili wapime kifua kikuu na watakaobainika waweze kupata tiba.
Dkt Isabela ametaja miongoni wa dalili za kifua kikuu ni pamoja na kupata homa za usiku, kukohoa damu ,joto kali la mwili nyakati za usiku, kukosa hamu ya kula kwa watoto .
Pia Dkt Isabela ametaja makundi ambayo yapo kwenye hatari zaidi ya kupata maambukizi ya kifua kikuu ni pamoja na watu wenye maambukizi ya magonjwa mengine kama vile Ukimwi, Kisukari, watu ambao wanafanya shughuli za uchimbaji madini.
No comments: