Na Jumbe Ismailly, SINGIDA
VIONGOZI wa vyama vya
siasa Mkoani Singida wameshauriwa kutoyapitisha majina ya wagombea wa nafasi
mbali mbali za uongozi katika vyama vyao watakaobainika kujihusisha na vitendo
vya ushirikina ili waweze kupata nafasi za uongozi walizoomba katika uchaguzi
mkuu ujao wa Raisi,Wabunge pamoja na Madiwani unaotarajiwa kufanyika mwezi
oktoba,mwaka huu.
Ushauri huo umetolewa na
Naibu Amiri JASUTA Mkoa wa Singida,Sheikh
Abdurahmani Hassani alipokuwa akiongea na waumini wa dini ya kiislamu
kwenye viwanja vya msikiti wa AL-FORUQAN,uliopo Kata ya Minga, Manispaa ya
Singida.
Aidha Naibu Amiri huyo
hata hivyo akawasisitiza pia waumini wa dini hiyo kutowachagua wagombea
wanaojihusisha na tamaa ya madaraka ya uongozi kupitia vitendo vya ushirikiana.
“Ikibainika mimi nasema
na ninashauri ikibainika kwamba mgombea ni mshirikiana na anafanya
makafara,anafanya ushirikiana asipewe kura hata moja akijulikana na akabainika
na zipo alama za mshirikina,mkimuoina anafanya vitu vya ajabu,anatoka usiku
anakwenda kuoga maji njiapanda
usiku”alisisitiza Naibu
Amiri huyo.
Aidha Naibu Amiri huyo
hata hivyo aliweka bayana kwamba endapo mgombea wa aina hiyo akibainika,vyama
vya siasa visipitishe jina lake kuendelea na mchakato wa kugombea kwenye nafasi
hiyo ya uongozi.
Alisema kiongozi huyo
kwamba viongozi wenye dhamira nzuri ya uongozi katika maeneo ya kata,jimbo na
nchi wawe ni watu wenye hofu ya mungu,wenye uchamungu na wenye imani na ambao
pia siyo wapagani kwa kutomwabudu mungu na badala yake wakawa wakimwanini shetani.
Masozi Abdala ni Amirati
katika msikiti wa Al-Shababu mjini Singida alibainisha kuwa idadi kubwa ya
wanawake wamekuwa wakiangamia kutokana na maadili wanayopendelea kuyatekeleza
kuwa yapo kinyume na maandiko ya mwenyezimungu katika maisha yao ya kila siku
Kwa mujibu wa Amirati
huyo akina mama wengi wanaangamia kutokana na vitendo vya ushirikana na upo
uwezekano mkubwa wa akina mama hao kuingia motoni kutokana na kujihusisha na
vitendo vya ushirikina kwa kutojiamini kwenye ndoa zao.
“Mwanamke yupo radhi
amuharibu mume wake lengo tu avutie kwamba mume aweze kumpenda hicho ndicho
kitu kikubwa sana kwa akina mama na kuwavutia wanaume ili watupende sisi kuliko
familia zao huo ni mtihani mkubwa sana”alifafanua Masozi.
Alibainisha Masozi kwamba
licha ya kwamba idadi kubwa ya wanawake wanaipenda dunia kuliko maarisho ya
mwenyezimungu,lakini wakumbuke kwamba hapa duniani ni mapito tu na hakuna mtu
atakayeishi milele na mwisho wa siku watakwenda kuulizwa.
Ili kukabiliana na
vitendo hivyo vya ushirikiana Amirati huyo alisisitiza kuwa kikibwa zaidi ni
kinamama kujitahidi kuitafuta elimu ya akhera kwa kwenda kwenye madrasa ili
waweze kujifunza ni nini kilichowaleta hapa duniani na kikubwa zaidi ya yote ni
kufanya ibada na hakuna zaidi ya hilo.
Akizungumzia suala la
mmomonyoko wa maadili,mmoja wa waumini wa msikiti wa Al-Forouqan,Ahmadi Daudi
Masilamba alisema tangu kituo cha Markasi kilipoanzishwa zaidi ya wanafunzi
1,000 wamepatiwa masomo yao ya dini na kwamba taarifa zilizopo ni wanafunzi
waliopitia katika Markasi hiyo wamekuwa wakifanya vizuri na wanaendelea kuwa
masheikh wazuri kwenye misikiti waliyopo.
MWISHO.


Post a Comment