Na AMINI NYAUNGO
Mamlaka ya mapato
Tanzania TRA Mkoa wa Singida wamepita katika maduka mbalimbali wakihimiza suala
la kulipa kodi pamoja na kusikiliza na kutatua changamoto za wafanyabiashara katika
maeneo yao ya Kazi.
Akizungumza mara baada ya
kutembelea wafanyabiashara hao meneja wa TRA Mkoa wa Singida Josephat Mwaipaja
amesema mwezi huu ni nimwezi wa kulipa kodi awamu ya pili hivyo wamepitia kuwakumbusha wafanyabiashara
kulipa kodi zao kwa wakati.
Amesema katika ziara yao
wamesikiliza na kutatua papokwa papo changamoto mbalimbali ambazo zilikuwa
zikiwakabili wafanyabiashara hao.
Katika hatua nyingine
Meneja Mwaipaja amewashukuru walipa kodi kwa kuendelea kuufanya mkoa wa Singida
kuvuka malengo katika suala la ukusanyaji wa Mapato.
Amesema lengo la mwaka ni
kukusanya bilion 30.54 ambapo kwa miezi kumi na moja walitakiwa kukusanya
shilingi bilioni 27.23 lakini mpaka sasa wamekusanya shilingi bilioni 29.79
ikiwa ni ufanisi wa asilimia 109.
Kwaupande wao baadhi ya
wafanyabiashara wamepongeza mamlaka ya mapato TRA kwa kuendelea kuwatembelea na
kutoa elimu ya mara kwa mara suala lililosaidia kuondoa changamoto.
Kwa upande wawafanyabiashara wameipongeza TRA mkoa waSingida kwa kuendelea kutoa elimu huku wakishirikiana vizuri
End
Post a Comment