JAMII IMETAKIWA KUACHA MILA POTOFU

Amini Nyaungo



Jamii imetakiwa kuenzi mila na desturi chanya zinazochangia ujenzi ambazo hulithishwa kutoka kizazi kimoja kwenda kingine.

Hayo ameyasema  Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii , Jinsia na Makundi Maalum, Amon Mpanju katika uzinduzi wa kitini cha majadiliano ya Mila desturi katika kijiji cha Ighombwe Mkoani hapa siku ya jana Juni 2,2025.



Akisema kuwa ni muhimu sana kwa jamii kuangalia tamaduni zilizochanya  ambazo zinafaida kwa jamii.



“Jamii inatakiwa kuangalia mila na tamaduni zilizokuwa sahihi katika jamii ili kuziendeleza na kulithishwa kwa jamii,” Mpanju



Kwa upande wa Katibu Tawala wa Wilaya ya Ikungi Rashid Mohamed Rashid amesema kuwa kupitia majadiliano hayo wananchi wamejua kuziacha mila potofu.



“Katika majadiliano haya yaliyofanyika jamii imejua mila potofu na kuziacha hivyo naamini itakuwa vyema kuziacha mara moja zile zisizokuwa sahihi,” Rashid



Aidha kwa upande wa wananchi ambapo walikuwa wanatoa mrejesho baada ya majadikiano wamesema mila mbaya ni pamoja na Chagulaga, Ukeketaji na kurithisha wake.

Mwisho

 

Post a Comment

Previous Post Next Post