SINGIDA KUZINDUA KAMATI YA USHAURI WA KISHERIA MAY 19 -RC SINGIDA

 


Na Robert Onesmo, Singida



MKUU wa Mkoa wa Singida Mhe.Halima Dendego, ametangaza kuzinduliwa kwa kamati ya Ushauri wa  kisheria ngazi ya Mkoa  itakayo zinduliwa rasmi May 19 2025  katika viwanja vya stendi ya zamani Mansapa ya Singida 


Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Dendego amesema kuwa kamati hiyo inayotarajiwa kuzinduliwa may 19 itaambatana na kliniki ya sheria bila malipo kwa wananchi wote Mkoa wa Singida 


Kwa upande mwingine Dendego ametoa rai kwa wananchi kujitokeza kwa wingi katika viwanja hivyo ili waweza kutibiwa kisheria katika mambo ambayo yawawatatiza.



Kwa mjibu wa Matrider Meckson ambaye ni Mkuu wa kitengo cha Sheria Mkoa wa Singida amesema zaidi ya wanasheria 50 watakuwepo  katika kliniki hiyo hivyo wananchi wanapaswa kujitokeza kwa wingi na kupata huduma hiyo bure.

Post a Comment

Previous Post Next Post