Na Sylvester Richard
Mkuu wa Mkoa wa Singida Mh. Halima Omary Dendego ametembelea Kaburi la Shujaa Liti ambaye ni Malkia wa kabila la Wanyuturu kwa lengo la kuhamasisha utalii wa ndani.Dendego amefanya ziara hiyo Aprili 27, 2025 akiambatana na viongozi mbalimbali wakiwemo viongozi wa vyombo vya ulinzi na usalama likiwemo Jeshi la Polisi, Jeshi la Magereza na zimamoto na uokoaji.
Aidha, akiwa kaburini hapo amewahamasisha wananchi wa Mkoa wa Singida na wageni wanaofika Mkoani Singida kusherehekea maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani (MEI MOSI) kufika kwenye kaburi la Shujaa huyo Mwanamke lililopo katika Kijiji cha Makuyu Singida pamoja na maeneo mengine yakiwemo makazi ya Mtemi Senge na Ziwa Kinda maeneo ambayo yanapatikana Manispaa ya Singida.


Post a Comment