Na Amini Nyaungo
Mkuu wa Mkoa wa Singida Halima Dendego amewaomba wakazi wa Singida wajiandae kwa fursa mbalimbali zitakazojitokeza wakati wa kupokea wageni zaidi ya elfu sita watakao kuja mkoani hapa kwa ajili ya Maadhimisho ya siku ya Wafanyakazi Duniani.
Dendego ameyasema hayo jana (March 26,2025)katika Iftar
iliyoandaliwa na Biostutain ambapo amesema kuwa wafanyabiashara wanatakiwa
wasilale wafanyekazi ipasavyo ili wanufaike na fursa hizo zitakazojitokeza za
ugeni huo.
" Kama unaendesha bodaboda basi endesha kweli, kama
unanyumba za wageni ziboreshe, kama hujasajili nyumba yako isajili ili wageni
hao wapate hifadhi na uweze kujipatia kipato.
Aidha ametumia nafasi hiyo kuwaomba kudumisha matendo mema
waliyoyafanya ndani ya mwezi mtukufu wa Ramadhani waendelee nayo hadi mwisho wa
maisha yao.
"Amani, upendo na ustaarabu ambao tumeutengeneza ndani
ya mwezi wa Ramadhani basi udumu katika maisha yetu ya kawaida baada ya mwezi
wa radhani," Dendego.
Mwisho

.jpg)
Post a Comment