MASTER JAY AKUBALI YAISHE KWA KIBA

 MASTER JAY AKUBALI YAISHE KWA KIBA

Na Amini Nyaungo

Mtayarishaji mkongwe wa muziki wa kizazi kipya nchini Tanzania Joachim Marunda Kimaryo (MASTER JAY) leo aomba kumaliza tofauti yake na Ali Kiba baada ya kuibuka mjadala ambao alimtuhumu msanii Ali Kiba kuwa miongoni mwa wabana pua.

Master Jay amemuomba radhi Kiba  leo katika kipindi cha Jirani kinachorushwa na Crown Media akisema kuwa hayakuwa maneno mazuri na alitumia kilevi wakati alipoongea maneno hayo.

Aidha ameweka wazi kuwa alitaka kumfuata Ali Kiba ili wayamalize na maisha mengine yaendelee kama ilivyokuwa huku akiweka wazi hana ugomvi wowote na Ali Kiba.

Katika usiku wa fainali ya BSS baada ya kutamatika Master Jay alihojiwa na chombo kimoja cha habari akisema kuwa Ali Kiba ni mbana pua hawezi kufananishwa na Bien kutoka Kenya ambaye anaimba muziki wa taratibu wa R&B.

MWISHO

 

Post a Comment

Previous Post Next Post