HABARI

MICHEZO

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

HABARI

HABARI

MAKALA

» » WANANCHI WAMESHIRIKISHWA KIKAMILIFU UJENZI WA BOMBA LA MAFUTA (EACOP)

 

Na Sylvester Richard.

Afisa Maawasiliano wa Mradi wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP) upande wa Tanzania Abass Abraham amesema kuwa wananchi wa Tanzania waliopitiwa na mradi huo wameshirikishwa kikamilifu katika kila hatua ikiwemo elimu juu ya uhifadhi wa mazingira, afya, fidia za nyumba na mashamba pamoja na elimu ya matumizi fedha.

Alisema hayo Juni 10, 2024 alipokuwa akitoa elimu kwa waandishi wa habari kutoka Klub ya wanahabari Mkoa Singida (SINGPRESS) katika ukumbi wa mikutano uliopo kwenye jengo la ofisi ya Mkuu wa Mkoa Singida.
Aidha, Abass amesema Mradi huo unahusisha nchi mbili ambazo ni Tanzania na Uganda na umeanza kutekelezwa 2016 huku ukiipitia Mikoa 8 ambayo ni Kagera, Geita, Shinyanga, Tabora , Singida, Dodoma, Manyara na Tanga.
Ameongeza kuwa, bomba hilo litakuwa na urefu wa Km. 1443 ambapo kwa upande wa Tanzania litakuwa na urefu wa Km. 1147 sawa na aslimia 80% na upande wa Uganda Km. 296 ambazo ni sawa na aslimia 20% . 

Akiongea juu ya fidia kwa watu waliopitiwa na mradi huo, amesema zaidi ya watu 9000 wamepitiwa na mpaka sasa asilimia 99 wamelipwa fidia ya kulipwa fedha au kujengewa nyumba.

Akiongea kuhusu mradi huo ndani ya Mkoa wa Singida Josephat Kanyunyu  ambaye ni Mratibu wa Mahusiano wa Mradi wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP) Mkoa wa Singida amesema mradi huo umepita Wilaya tatu ambazo ni Iramba, Mkalama na Singida huku watu 1296 wakiguswa na mradi huo.

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Leave a Reply